Cybercrimes Act
__________________________________________________________________
(b) baada ya kupata uelewa kuhusiana na taarifa zilizo kinyume na sheria kwa
namna nyingine zaidi ya amri ya mamlaka ya umma, haraka iwezekanavyo
ataitaarifu mamlaka husika.
Mtoa huduma
ya utafutaji wa
taarifa
Notisi ya
kuondoa
44.-(1) Mtoa huduma ya utafutaji wa taarifa hatawajibika kwa matokeo ya
utafutaji huo, kwa masharti kwamba(a) haanzishi mawasiliano;
(b) hachagui mpokeaji wa mwasiliano; na
(c) hachagui au kubadilisha taarifa iliyoko kwenye mawasiliano.
(2) Kwa madhumuni ya kifungu hiki, “mtoa huduma ya utafutaji wa taarifa”
maana yake ni mtu anayetengeneza au anayeendesha huduma ambayo inatafuta taarifa
inayotengeneza kiashiria inayohusiana na taarifa za mtandao au anawezesha
upatikanaji wa vifaa vya kielektroniki kwa ajili ya utafutaji wa taarifa inayotolewa na
mtu mwingine.
45.-(1) Mtu anaweza, kupitia notisi ya kuondoa kumtaarifu mtoa huduma(a) kuhusiana na data au taarifa iliyomnyima mpokeaji au mtu wa tatu haki ya
huduma;
(b) vitu au shughuli ambayo ni kinyume cha sheria; au
(c) suala lolote linalotekelezwa au linalotolewa kinyume cha sheria hii au
sheria nyingine.
(2) Kwa madhumuni ya sehemu hii, notisi ya kuondoa itakuwa katika hali ya
kudumu ikitumwa na mlalamikaji kwenda kwa mtoa huduma au wakala wake na
itajumuisha(a) jina kamili na anuani ya mlalamikaji;
(b) saini ya mlalamikaji;
(c) maelezo ya haki inayodaiwa kuvunjwa;
(d) maelezo juu ya shughuli ambayo inadaiwa kuwa chimbuko la kitendo
kilicho kinyume cha sheria;
(e) hatua ya utatuzi inayotakiwa kuchukuliwa na mtoa huduma kuhusiana na
lalamiko;
(f) maelezo kuwa mlalamikaji anatenda kwa nia njema;
(g) maelezo ya mlalamikaji kuwa, kwa ufahamu wake, taarifa iliyomo kwenye
taarifa zilizochukuliwa ni sahihi.
(3) Mtu anayewasilisha taarifa kwa mtoa huduma kuhusiana na muamala usio
50