Cybercrimes Act
__________________________________________________________________
(c) maelezo ya hatua zinazokusudiwa kuchukuliwa, madhumuni, kiasi na
muda wa matumizi unaokusudiwa.
(3) Afisa utekelezaji wa sheria atahakikisha kuwa mabadiliko yaliyofanywa
kwenye mfumo wa kompyuta au data iliyomo kwenye kompyuta kuhusiana na
mtuhumiwa zinajikita kwenye marekebisho yaliyo ya msingi kwa ajili ya uchunguzi
na kwamba mabadiliko yanafanywa baada ya kukamilika kwa uchunguzi.
(4) Wakati wa uchunguzi, afisa utekelezaji wa sheria ataingiza:
(a) mbinu za kiufundi zilizotuimika, muda na terehe ya maombi;
(b) utambuzi wa mfumo wa kompyuta na maelezo ya mabadiliko
yaliyofanyika wakati wa uchunguzi;
(c) taarifa yoyote iliyopatikana;
(5) Taarifa iliyopatikana italindwa dhidi ya mabadiliko, kufutwa bila ya
idhini na kuigia kwenye mfumo bila idhini.
(6) Idhini iliyotolewa chini ya kifungu kidogo cha (1) itakuwa halali kwa
kipindi cha siku kumi na nne.
(7) Mahakama inaweza, kufuatia maombi, kuongeza muda uliotolewa chini ya
kifungu kidogo cha (6) kwa kipindi kingine cha siku kumi na nne au kwa kipindi
kingine kwa kadri itakavyoona inafaa.
(8) Iwapo mchakato wa uwekaji wa kifaa unahitaji kutembelea eneo, masharti
ya kifungu cha 30 yatatumika.
(9) Pamoja na amri iliyotolewa chini ya kifungu kidogo cha (1), mahakama
inaweza, kufuatia maombi, kumuamuru mtoa huduma awezeshe mchakato wa
kuweka kifaa.
(10) Waziri anaweza, kwa Taarifa itakayochapishwa kwenye Gazeti la
Serikali, kuainisha makosa chini ya Sheria hii ambayo mahakama inaweza kutoa amri
ya kutumia kifaa cha TEHAMA katika uchunguzi.
Usikilizaji wa
maombi
38. Utaratibu wa kusikiliza maombi chini ya Sehemu hii utafanywa kwa
upande mmoja na kwa siri.
SEHEMU YA TANO
WAJIBU WA MTOA HUDUMA
Kutowajibika
kufanya
ufuatiliaji
39.-(1) Wakati wa kutoa huduma chini ya Sehemu hii, mtoa huduma(a) hata wajibika kufuatilia data ambayo anaisambaza au kuhifadhi;
(b) tafuta maelezo au mazingira yanayoashiria shughuli zinazofanywa
47