Cybercrimes Act
__________________________________________________________________
(a) anawasilisha, anafichua au anasambaza data kompyuta, programu ya
kompyuta, ishara ya kuingilia au agizwa kwa mtu ambaye hajaidhinishwa;
(b) anapokea data kompyuta ambayo haijaidhinishwa,
ametenda kosa na akitiwa hatiani, atawajibika, kulipa faini ya kiasi ambacho ni
kikubwa kati ya kiwango kisichopungua shilingi milioni mbili au mara tatu ya
thamani ya faida iliyopatikana kinyume cha sheria, au kutumikia kifungo kwa kipindi
kisichopungua mwaka mmoja au vyote.
(3) Mtu ambaye isivyo halali na kwa makusudi anaharibu au anabadili data
yoyote ya kompyuta, iwapo data hiyo inatakiwa kutunzwa kisheria au ni ushahidi
kwenye shauri lolote chini ya Sheria hii kwa(a) kuondoa au kubadilisha data, programu au taarifa nyingine yoyote iliyoko
ndani au nje ya mfumo wa kompyuta;
(b) anawasha, anaingiza au anapakua programu ambayo imetengenezwa kwa
lengo la kuondoa au kubadilisha data, programu au aina yoyote ya taarifa
ilioyoko ndani au nje ya mfumo wa kompyuta; au
(c) anatengeneza, anabadilisha au anaharibu namba ya siri, namba binafsi ya
utambulisho au namna inayotumika kuingika kwenye mfumo wa
kompyuta,
atakuwa ametenda kosa na akitiwa hatiani, atawajibika kulipa faini ya kiasi ambacho
ni kikubwa kati ya kiwango kisichopungua shilingi milioni ishirini au mara tatu ya
thamani ya faida iliyopatikana kinyume cha sheria, au kutumikia kifungo kwa kipindi
kisichopungua miaka mitano au vyote.
Ujasusi data
Sura ya 47
Kuingilia
mfumo
kinyume cha
sheria
8.-(1) Bila kuathiri masharti ya sheria ya Usalama wa Taifa, mtu hataingilia
pasipo idhini na kujipatia data kompyuta iliyokingwa dhidi ya kuingiliwa.
(2) Mtu akatayekiuka kifungu kidogo cha (1) atakuwa ametenda kosa na
akitiwa hatiani, atawajibika kulipa faini ya kiasi ambacho ni kikubwa kati ya kiwango
kisichopungua shilingi milioni ishirini au mara tatu ya thamani ya faida iliyopatikana
kinyume cha sheria, au kutumikia kifungo kwa kipindi kisichopungua miaka mitano
au vyote
9. Mtu ambaye, kinyume cha sheria na kwa makusudi anazuia au anaingilia(a) utendaji kazi wa mfumo wa kompyuta;
(b) matumizi au uendeshaji wa mfumo wa kompyuta,
atakuwa ametenda kosa na akitiwa hatiani, atawajibika kulipa faini ya kiasi ambacho
37