Cybercrimes Act __________________________________________________________________ _____ TAARIFA _____ Muswada huu utakaowasilishwa Bungeni umechapishwa pamoja na madhumuni na sababu zake kwa ajili ya kutoa taarifa ya jumla kwa umma. Dar es Salaam, 3 Februari, 2015 OMBENI Y. SEFUE Katibu wa Baraza la Mawaziri MUSWADA wa Sheria inayoainisha makosa yanayohusiana na matumizi ya mfumo wa kompyuta na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, kuweka utaratibu wa upelelezi, ukusanyaji na matumizi ya ushahidi wa kielektroniki na masuala mengine yanayohusiana na hayo. IMETUNGWA na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. SEHEMU YA KWANZA MASHARTI YA AWALI Jina na tarehe ya kuanza kutumika 1. Sheria hii itaitwa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015. Sheria hii itaanza kutumika tarehe ambayo Waziri ataiteua na kuitangaza katika Gazeti la Serikali. Matumizi 2. Isipokuwa kwa kifungu cha 50, Sheria hii itatumika Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar. Tafsiri 3. Katika sheria hii, isipokuwa kama muktadha utahitaji vinginevyo“kuingia” kuhusiana na mfumo wa kompyuta maana yake ni kuingia, kutoa maelekezo, kuwasiliana, kuhifadhi data au kupokea data kutoka katika mfumo wa kompyuta au vinginevyo kutumia rasilimali zozote za mfumo wa kompyuta au 32

Select target paragraph3