Cybercrimes Act
__________________________________________________________________
(4) Mtu anayemiliki au mwangalizi wa mfumo wa kompyuta anaweza
kumuomba afisa utekelezaji wa sheria ruhusa ya kuingia au kudurufu taarifa zilizopo
kwenye mfumo wa kompyuta baada ya ukamataji wa mali.
(5) Bila kuathiri masharti ya kifungu kidogo cha (4), afisa utekelezaji wa
sheria anaweza kukataa kuruhusu kuingia kwenye mfumo au kudurufu taarifa iwapo
anazo sababu za msingi za kuamini kuwa kuruhusu kuingia au kudurufu taarifa(a) itakuwa ni kosa; au
(b) kutaathiri(i)
uchunguzi unaohusiana na upekuzi
(ii)
upelelezi mwingine unaoendelea; au
(iii) shauri lolote lililopo mahakamani au ambalo linaweza
kufunguliwa kuhusiana na uchunguzi huo.
(6) Katika kifungu hiki “eneo” inajumuisha ardhi, majengo au chombo cha
usafiri.
Utoaji data
32.-(1) Pale ambapo data inanitajika kuwekwa wazi kwa madhumuni ya
uchunguzi wa kijinai au kuendeshwa kwa kesi mahakamani, Askari Polisi Mkuu wa
kituo au afisa mtekelezaji wa sheria mwenye cheo cha askari mkuu wa kituo anaweza
kutoa amri kumtaka(a) mtu yeyote kuwasilisha data iliyoainishwa ambayo mtu huyo anaimiliki au
iliyo chini ya uangalizi wake ambayo imehifadhaiwa kwenye mfumo wa
kompyuta; au
(b) mtoa huduma yeyote, kuwasilisha taarifa kuhusiana na mteja zilizo
kwenye umiliki au uangalizi wake.
(2) Iwapo kitu chochote kinachohusiana na upelelezi kinajumuisha data
iliyohifadhiwa kwenye mfumo wa kompyuta au kwenye kifaa, amri itachukuliwa
kumtaka mtu kutoa au kuruhusu upatikanaji wa data hiyo katika namna ambayo
inasomeka na inayoweza kuondolewa.
Utunzaji data
wa dharura
33. Pale ambapo Askari Polisi Mkuu wa kituo au afisa utekelezaji wa sheria
anazo sababu za kuamini kuwa data kompyuta ambayo inahitajika kwa madhumuni
ya uchunguzi inaweza kupotea au kubadilishwa, anaweza kutoa amri itakayomtaka
mtu mwenye uangalizi au umiliki wa kifaa au data kompyuta kuitunza kwa kipindi
kisichozidi siku kumi na nne.
Utoaji na
34.-(1) Pale Askari Polisi Mkuu wa kituo au afisa mtekelezaji wa sheria
45