Cybercrimes Act
__________________________________________________________________
“afisa utekelezaji wa sheria” maana yake ni afisa wa polisi mwenye cheo cha Mkaguzi
Msaidizi wa Polisi, mpelelezi, afisa Usalama wa Taifa mwendesha mashtaka au
mtu aliyeidhinishwa chini ya sheria yoyote;
“Waziri” maana yake ni Waziri anayehusika na masuala ya TEHAMA.
“kuchapisha” maana yake ni
usambazaji, uwasilishaji, uwekaji wazi,
kubadilishana,uchapishaji, au usambazaji wa aina yoyote ile;
“mali” maana yake ni mali ya aina yoyote, inayogusika au isiyo gusika na inajumusha:
(a) fedha yoyote inayotumika au isiyotumika katika Jamhuri ya Muungano
Tanzania;
(b) taarifa, ikijumuisha programu, data au nakala zake, zinazoweza kusomwa
na binadamu au kwa kompyuta; au
(c) haki yoyote au maslahi kwenye mali;
“ubaguzi” maana yake ni taarifa za namna yoyote zinazokuza au kuchochea chuki,
ubaguzi au vurugu dhidi ya mtu au kundi la watu kwa msingi wa tabaka, rangi,
asili,utaifa, kabila au dini;
“mtoa huduma” maana yeke ni mtu au upande unaowezesha mfumo wa taarifa
kupatikana kwa mtu-kati.
SEHEMU YA PILI
MASHARTI YANAYOHUSIANA NA MAKOSA NA ADHABU
Kuingia
kinyume cha
sheria
4.-(1) Mtu hataingia au kusababisha kuingiliwa mfumo wa kompyuta kinyume
cha sheria na kwa makusudi.
(2) Mtu akatayekiuka kifungu kidogo cha (1) atakuwa ametenda kosa na
akitiwa hatiani, atawajibika kulipa faini ya kiasi ambacho ni kikubwa kati ya kiwango
kisichopungua shilingi milioni tatu au mara tatu ya thamani ya faida iliyopatikana
kinyume cha sheria, au kutumikia kifungo kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja
au vyote.
Matumizi ya
mfumo wa
kompyuta
kinyume cha
5.-(1) Mtu hatatumia au kuendelea kutumia mfumo wa kompyuta, kinyume
cha sheria na kwa makusudi, baada ya kuisha kwa muda ambao aliruhusiwa kutumia
mfumo wa kompyuta.
35