Cybercrimes Act __________________________________________________________________ ukusanyaji wa data nyendo Utoaji na ukusanyaji wa maudhui katika data Amri ya mahakama Matumizi ya kifaa cha TEHAMA katika uchunguzi mwenye cheo cha askari mkuu wa kituo anaridhika kuwa data kompyuta inahitajika kwa madhumuni ya uchunguzi, afisa huyo anaweza kutoa amri kwa maandishi kwa ajili ya(a) ukusanyaji au kuweka kumbukumbu za taarifa za kompyuta zinazohusiana na mawasilano maalum kwa kipindi maalum; au (b) kumruhusu na kumsaidia afisa utekelezaji wa sheria kukusanya na kuweka kumbukumbu za data hizo. (2) Kwa madhumuni ya kifungu hiki “data nyendo” maana yake ni taarifa: (a) inayohusiana na mawasiliano kwa mfumo wa kompyuta; (b) iliyotolewa na mfumo wa kompyuta ambao ni sehemu ya mlolongo wa mawasiliano; na (c) inayoonesha chanzo cha mawasiliano,njia iliyotumika, muda,ukubwa, uelekeo na aina ya huduma zinazoambatana nazo. 35. Pale ambapo Askari Polisi Mkuu wa kituo au afisa mtekelezaji wa sheria mwenye cheo cha askari mkuu wa kituo anazo sababu za msingi za kushuku au kuamini kuwa yaliyomo kwenye mawasiliano ya kielektroniki yanahitajika kwa madhumuni ya uchunguzi, anaweza kutoa amri ya: (a) kukusanya, kurekodi, kuruhusu au kuisaidia mamlaka husika kukusanya au kurekodi taarifa zilizomo kwenye inayohusishwa na mawasiliano maalum yaliyotolewa ka njia ya mfumo wa kompyuta; au (b) kumuidhinisha afisa utekelezaji wa sheria kukusanya au kurekodi data kwa kupitia njia ya kiufundi. 36. Pale ambapo utoaji data au utunzaji data wa dharura chini ya vifungu vya 31, 32, 33, 34 au 35 kwa kadri itakavyokuwa, hauwezi kufanyika bila kutumia nguvu au kutokana na pingamizi kutoka kwa mtu mwenye kumiliki data au thamani ya ushahidi katika data inaweza kuhifadhiwa kwa amri ya mahakama, afisa mtekelezaji wa sheria anaweza kuomba mahakamani amri ya utoaji au utunzaji wa data. 37.-(1) Pale ambapo afisa utekelezaji wa sheria anaridhika kuwa ushahidi wa msingi hauwezi kukusanywa kwa kutumia utaratibu uliainishwa chini ya Sehemu hii, afisa utekelezaji huyo anaweza kuiomba mahakama kutoa amri ya kuidhinisha matumizi ya kifaa cha uchunguzi. (2) Maombi yaliyotolewa chini ya kifungu kidogo cha (1) yatajumuisha(a) jina na anuani ya mtuhumiwa; (b) maelezo ya mfumo wa kompyuta unaolengwa; na 46

Select target paragraph3