Cybercrimes Act __________________________________________________________________ sheria Kuingilia mawasiliano kinyume cha sheria (2) Mtu akatayekiuka kifungu kidogo cha (1) atakuwa ametenda kosa na akitiwa hatiani, atawajibika kulipa faini ya kiasi ambacho ni kikubwa kati ya kiwango kisichopungua shilingi milioni moja au mara tatu ya thamani ya faida iliyopatikana kinyume cha sheria, au kutumikia kifungo kwa kipindi kisichopungua miezi sita au vyote. 6.-(1) Mtu ambaye, kinyume cha sheria na kwa makusudi(a) anaingilia kwa kutumia njia ya kiufundi au kwa njia nyingine yoyote: (i) mawasilano yasiyo ya umma kwenda au kutoka au yaliyo ndani ya mfumo wa kompyuta; (ii) mawasiliano yasiyo ya umma ya kieletromaniginetiki yakokayo katika mfumo wa kompyuta usio wa umma; au (iii) mfumo wa kompyuta usio wa umma ambao umeunganishwa na mfumo mwingine wa kompyuta. (b) anakwepa hatua za udhibiti zilizoelekezwa kwa ajili ya kukinga kuingiliwa kwa maudhui yaliyomo kwenye mawasiliano yasiyo ya umma. (2) Mtu atakayekiuka kifungu kidogo cha (1) atakuwa ametenda kosa na akitiwa hatiani, atawajibika kulipa faini isiyo pungua shilingi milioni tano au kutumikia kifungo kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja au vyote. Kuingilia data kinyume cha sheria 7.-(1) Mtu ambaye, kinyume cha sheria na kwa makusudi(a) anaharibu au anazorotesha data kompyuta; (b) anafuta data kompyuta; (c) anabadili data kompyuta; (d) anaifanya datamkompyuta ipoteze maana, ishindwe kutumika au ikose ufanisi; (e) anazuia au anaingilia matumizi halali ya data kompyuta; (f) anazuia au anamuingilia mtu mwingine anayetumia data kompyuta kihalali; au (g) anamzuia mtu aliyeidhinishwa kutumia data kompyuta, atakuwa ametenda kosa na akitiwa hatiani, atawajibika kulipa faini ya kiasi ambacho ni kikubwa kati ya kiwango kisichopungua shilingi milioni kumi au mara tatu ya thamani ya faida iliyopatikana kinyume na sheria au kutumikia kifungo kwa kipindi kisichopungua miaka mitatu au vyote. (2) Mtu ambaye- 36

Select target paragraph3